Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mr. T Touchez hawezi kuniangusha - Nay

Ijumaa , 17th Feb , 2017

Msanii wa muziki wa hip hop bongo Emmanuel Elibariki a.k.a 'Nay wa Mitego' amesema hawezi kushuka kimuziki kwa kuachana na producer Mr. T Touchez na kusema kuwa hajawahi kuanguka katika muziki wake kutokana na maneno  ya watu wanaomuombea mabaya.

Amefunguka hayo wakati akijibu maswali ya watu katika kipindi cha KIKAANGONI kinachoruka LIVE kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV ambapo kuwa walitoa maoni yao kuwa ameshuka kimuziki baada ya kuachana na aliyekuwa producer wake Mr. T Touchez.

Amesema kuwa hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kubadilisha upepo wa muziki wake na kwamba yeye anamuamini Mungu wake ambaye anapatia riziki, na kuongeza kuwa hashangazwi na maneno hayo kwa kuwa huwa hana bahati ya kusemwa kwa mazuri pindi anapokuwa karibu na mtu na baadaye kuachana naye, iwe kimapenzi au kikazi.

"Siwezi kushuka kwa ajili ya maneno ya watu na mimi na kwa sababu mimi ninamuamini Mungu wa dunia yangu ambaye kila nikimuomba ananijibu kwa wakati. Pia mimi siyo msanii aliyedumaa hivyo hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kubadilisha upepo wa muziki wangu. Si mnaona sijiwezi inakamata Top 10 vituo mbalimbali hivyo sijashuka kimuziki". Alisema Nay wa Mitego

Nay wa Mitego akiwa KIKAANGONI

Nay ameongeza kuwa katika kipindi chote alichokuwa akifanya kazi na Mr. T Touchez alikuwa akimthamini kama producer ambaye anastahili kufanya kazi katika mazingira mazuri ndiyo maana hata kazi nyingine zilizokuwa zikifanyika katika studio yake ya Free Nation hakuwahi kumdai pesa yoyote ya kazi hizo.

 Aidha Nay ameeleza kuwa hana kinyongo na producer wake huyo ambaye walikwaruzana zaidi ya miezi sita iliyopita huku akiwa amegoma kueleza chanzo cha ugomvi wao na producer huyo aliyemuandalia 'hits' kadhaa.

"Sina kinyongo na Mr.T Touchez hata kidogo nipo tayari kufanya naye kazi kama akisema kwa sababu siwezi kuishi kwa kulipiziana visasi, na wala siwezi kujibizana naye, maana baba hawezi kujibiana na mtoto" alisema Nay.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali