Jumatano , 22nd Jul , 2015

Mbunge wa Mbeya Mjini na msanii wa muziki Joseph Mbilinyi, maarufu kama Mr. Sugu ameelezea kujivunia kipindi chake cha miaka 5 bungeni.

Mbunge wa Mbeya Mjini Mh. Joseph Mbilinyi aka Sugu

Hii imekuja baada ya lawama na fikra za wengine kuwa amekuwa na mchango mdogo tu katika kuipigania sanaa kwa nafasi aliyopata.

Mr. Sugu ameeleza hayo na kusisitiza kuwa, hakuwa mbunge wa wasanii bali mbunge wa Mbeya, akieleza kuwa, kama msanii hakuwa anajituma na kazi yake, ni lazima abakie kuwa mtu wa lawama mara zote.