Jumatatu , 7th Jan , 2019

Msanii nguli wa muziki wa Marekani, Robert Kelly maarufu kama R. Kely, amekuwa kwenye wakati mgumu baada ya filamu inayoelezea maisha yake kuanza kurushwa hewani, huku ikionesha ukatili wa kingono aliokuwa akiwafanyia mabinti wadogo na baadhi ya wafanyakazi wa kike.

Filamu hiyo ambayo ni mtitiriko wa vipindi kadhaa, imewashtua raia wa Marekani wakiwemo wasanii wenzake, ambao walionesha kutofurahishwa nayo, na kutoa maoni yao ambayo huenda yakamuweka pabaya msanii huyo mwenye sauti ya kipekee duniani.

Miongoni mwa wasanii ambao wamezungumzia hilo ni John Legend ambaye alikubali pia kuonekana kwenye filamu, amesema anawaamini wanawawake hao na kwamba R. Kelly amewaumiza watu wengi kwenye maisha yao.
 

Neyo naye alifunguka ya moyoni na kuandika kwamba kitendo cha R. Kelly kufanya vitendo hivyo ni vitu ambavyo haviwezi kukubalika, kwani ni muhimu kuwalinda watoto zaidi kuliko kuulinda muziki.

Rapper Meek Mill naye amesema baada ya kuangalia filamu hiyo ametokea kuchukizwa na R. Kelly, kwani anaamini kila kilichozungumzwa.

UTATA WAIBUKA JUU YA TUHUMA

Baada ya back vocal singer wa R. Kelly, Jovante Cunningham kusema kuwa R. Kelly alishawahi kufumaniwa akifanya ngono na marehemu Aaliyah kwenye basi la tour, mama mzazi wa Aaliyah BI. Diane Haughton alikanusha taarifa hiyo na kusema kwamba wao kama wazazi walikuwa bega kwa bega na mtoto wao kwenye ziara zake zote, na haijawahi tokea tukio hilo.

Ikumbukwe kwamba R. Kelly na Aaliyah walidaiwa kuoana kwa siri wakati Aaliya akiwa na miaka 15, hivyo walifoji vyeti aonekane ana miaka 18, jambo ambalo wenyewe walilikanusha kila walipohojiwa, na ndio ikawa chanzo cha marehemu Aaliyah kutopenda kuweka maisha yake binafsi kwenye mitandao.

 

URGENT MESSAGE Hi Team Aaliyah, it has come to our attention that Aaliyah's mother Diane Haughton has reached out to a fan as a call to action for the Special Ones (As she so lovingly calls us) with this direct quote in response to the Lifetime Surviving RKelly Documentary . . Please forward this message and quote to any media outlet, anyone and everyone you know via all your social media platforms, websites, blogs etc... It is urgent that we do this ASAP as the documentary is set to air on the 3rd of January . . Aaliyah isn't here to defend herself. We as a fanbase are, and we must defend her now! . We can't let "LIEtime" get away with this defamation of character on Aaliyah, her family, her estate, her foundation. We have the power in 2019 via social media to squash this story once and for all! Make it go viral! .Let’s do this! Anyone need the quote for reposting or media purposes DM Image & some wording in the body of this post reposted from @aaliyah_archives . #Aaliyah #aaliyahdanahaughton #aaliyahhaughton #TeamAaliyah #RKelly #lifetime #bet #foxnews #theshaderoom #lifetimetv #balleralert #thesource #thesourcemagazine #peoplemagazine #missyelliott #mediatakeout #wendywilliams #vh1 #mtv #pressrelease #urbanmedia #xxlmagazine #complexmag #complexmagazine #vibemagazine #vox #newsweek

A post shared by Aaliyah For MAC (@aaliyahformac) on

Licha ya hayo, wasanii wakubwa kama Jay Z na Lady Gaga, wamekataa kuonekana kwenye filamu hiyo, ambayo inaaminika na wengi kuwa imetengenezwa ili kummaliza R.Kelly kimuziki.

Ikumbukwe kwamba miaka ya 2002 hadi 2007, R. Kelly aliwahi kutuhumiwa kuwadhalilisha kingono baadhi ya wanawake hadi kupandishwa kizimbani, baada ya kuonekana kwa video akimkojolea mwanamke, na mwingine kudai kuwa alimuambukiza ugonjwa wa zinaa, na mashtaka mbali mbali ya kujihusisha kingono na wasichana ambao wako chini ya umri, kesi zote hazikumtia hatiani na kumuacha huru.

Baada ya kuachwa huru kutokana na tuhuma hizo, R. Kelly aliandika nyimbo mbali kali zilizofanya poa zaidi, ikiwemo alum ya Happy People na Yoo Saved me, ambayo wengi waliamini ni shukrani yake baada ya kunusurika kufungwa.

Hata hivyo baadhi ya watu nchini Marekani wameonesha kusikitishwa na kuchukizwa na malalamiko juu ya R. Kelly, wakiamini kwamba malalamiko yao hayatiliwi maanani kutokana na ubaguzi wa rangi, kwani katika matukio yote anayolalamikiwa kuyafanya, hakuna lililotolewa na binti mweupe.