Jumamosi , 10th Jan , 2015

Katika kuelekea kwenye mashindano makubwa kabisa ya soka ya African Cup of Nations kwa mwaka huu, msanii wa Uganda Eddy Kenzo kwa mujibu wa taarifa za awali amechaguliwa kushiriki katika project kubwa ya wimbo rasmi wa mashindano hayo.

Eddy Kenzo

Eddy Kenzo atakuwa ni msanii pekee kutoka Afrika Mashariki kushiriki katika kazi hii akiwakilisha wengine wote kutoka nchi Tano za eneo hili, nafasi ambayo ni ya heshima ya kipekee kwa sanaa yake.

Eddy Kenzo ambaye ngoma yake ya Sitya Loss imeweza kumpatia umaarufu zaidi Afrika, kwa shavu hili anakuwa ni moja kati ya wasanii ambao mwaka huu kwao ukiwa mwanzoni kabisa, tayari umeonesha nuru ya mafanikio makubwa.

Tags: