Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kashfa zamrudisha Shigongo darasani

Jumapili , 13th Aug , 2017

Mtunzi wa vitabu mashuhuri Tanzania Erick James Shigongo, anatarajia kurudi shule na kusoma elimu ya shahada, baada ya kuhangaika muda mrefu kutafuta nafasi hiyo, huku akisukumwa na masimango na matusi ya mitandaoni.

Erick Shigongo

Kwenye ukurasa wake wa facebook Erick Shigongo ameandika waraka mrefu akielezea safari yake kitaaluma na furaha aliyonayo, ya kuweza kufikia ndoto yake ya kuwa na elimu ya chuo kikuu, licha ya kuwa na mafanikio makubwa kwenye kazi zake za utunzi na maisha kiujumla.

"Ndoto imetimia, hatimaye naingia Chuo Kikuu, nikiwa mtoto nilitamani sana kusoma hadi chuo kikuu lakini sababu ya umasikini na mazingira magumu hasa shule nilizosoma, sikufaulu mtihani wa darasa la saba, nikarudia darasa la saba katika shule nyingine lakini bado sikufaulu, nilijiona mjinga! Nikajaribu kupitia njia ya 'vikozi' vidogo ili hatimaye niingie chuo kikuu lakini sikufanikiwa, nikaachana na ndoto hiyo na kuanza ujasiriamali", aliandika Erick Shigongo.

Erick Shigongo alendelea kuandika akisema kuwa ndoto yake hiyo imefanikiwa baada ya kujiunga na mfumo wa RPL ambao walifanya watu wenye uzoefu auwaliofanya mambo fulani katika jamii bila kuwa na elimu, na kuwapa nafasi ya kusoma elimu ya juu, ndipo alifanikiwa kupata mwaka huu, baada ya mwaka jana kufeli.

"Nikakusanya vitabu vyangu ambavyo nimekwishaandika na kuvipeleke Tume ya Vyuo Vikuu na kuomba niruhusiwe kufanya mtihani huo, nikaruhusiwa, mwaka jana nikafanya na kufeli, sikukata tamaa, mwaka huu nikafanya tena na kufaulu, hivyo mwezi wa tisa ninaanza mwaka wa kwanza ", aliandika Erick Shigongo.

 

HABARI ZAIDI

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu

Mwili wa Boaz Sanga, Mwanafunzi wa CHuo cha SAUTI Mwanza baada ya kupatikana Pembezoni wa Ziwa Viktoria

Mwanafunzi wa SAUTI afariki akijaribu kuogelea