
Kartel amethibitika kuhusika na tukio la kuua kwa kumshambulia na kumpiga Marehemu Lizard akishirikiana na wenzake watano, ambao wote kwa pamoja watafika mahakamani tarehe 27 mwezi huu kwa ajili ya kusomewa hukumu yao.
Tukio hili limetokea kugusa watu wengi katika ngazi ya kimataifa, wakiwepo mastaa wakubwa hasa kutokana na umahiri wa Vybz Kartel katika jukwaa la muziki wa kimataifa, ambapo amekwishafanya kazi na mastaa kama vile Pitbull, Missy Elliott, Rihanna kati ya wengineo.