Jumanne , 18th Mar , 2025

Huenda kukawa na kutambulishwa kwa msanii mpya kutoka kwa Music Recording Label ya Wcb Wasafi iliyo china ya msanii Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz

Pichani ni Msanii Diamond Platnumz

Taarifa hii imetolewa na msanii Diamond katika insta story yake ambapo amepost mkataba ukionesha kusaini kwa msanii mpya katika label hiyo ambaye huenda akatambulishwa siku za hivi karibuni ikiwa tu ni wiki kadhaa zimepita tangu msanii Mbosso kutangaza kutoka katika label ya Wcb Wasafi

Utakumbuka ni wiki kadhaa zimepita tangu msanii Diamond kuweka wazi kutafuta wasanii watano wapya ambao atawasaini katika label hiyo na huenda huyo akawa ni mmoja kati ya wale watano aliyowaongelea msanii huyo.