Jumapili , 23rd Mei , 2021

Baada ya ukimya wa takribani miezi 10 bila kuachia kazi yoyote, Dayna Nyange (Dragon Queen) sasa kurejea na Extended Play (EP) inayoitwa 'ELO' ambayo alikuwa akiiandaa kwa kipindi cha miezi 6.

Msanii Dayna Nyange

Akiwa jijini Lagos nchini Nigeria kwa shughuli zake mbalimbali ikiwa ni pamoja na muziki, Dayna amethibitisha kukamilika kwa projects zake kibao ikiwa ni pamoja na EP yake ambayo itakuwa ya kwanza kupitia mahojiano ‘’Moments With Dayna Nyange’’ huku kukiwa na collabo za ndani na kimataifa za kutosha.

Star huyo aliyewahi kutikisa kupitia kazi zake kama ‘Komela, Mafungu ya nyanya’ muda wowote ataweka wazi cover ya EP na tracklist.