Jumanne , 27th Jan , 2026

Staa wa Muziki ndani na nje ya Africa Davido amemuomba mke wake Chioma kumpa ruhusa ya kufanyiwa Masaji na wanawake 10 tofauti!

Picha ya Davido na mkewe Chioma

Davido ameomba hilo kwa mkewe kufuatia Mwanamitandao maarufu iShowSpeed kutrend akionekana akifanyiwa huduma ya masaji na warembo 10 nchini Ghana.

Insta Story ya Davido amepost video ikimuonyesha iShowSpeed na wanawake hao na kuandika 

“Chioma Mke wangu kipenzi naomba uniruhusu, hii ni Ghana" 

iShowSpeed amemaliza ziara yake ya kutembelea nchi 20 barani Africa kama Algeria,Misri, South Africa, Kenya, Ghana, Côte d’Ivoire, Zambia, Rwanda, Nigeria.