Picha ya Idris Sultan
Idris Sultan amehoji taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter ambapo ameandika kuwa
"Siku hizi tukipata watoto tu cha kwanza ni IG Account, Bank Account atajijua mwenyewe, 'likes' za ndugu zetu zitawasomesha nadhani, hapo tunawapa presha kuwa ni lazima kuiendeleza hiyo 'page' wakikua, itakuaje kama hawataki mitandao ya kijamii wanataka kuwa maspai".
Aidha baada ya post hiyo msanii mkongwe wa HipHop AY, nae alishea comment kuhusiana na hilo kwa kuandika "Halafu Akaunti ya mtoto ina-post 'i love you dad' pia una-comment 'i love you too son au daughter' ni ujinga".