.jpg?itok=Wc3OCoYz×tamp=1546671409)
Alikiba.
Domo Kaya amefunguka hayo kupitia FRIDAY NIGHT LIVE ya EATV, ambapo amesema kuwa Alikiba kutumia neno hilo sio vibaya lakini alitakiwa kuomba ruhusa kwanza kwake.
"Nawasihi wadogo zetu kuwa wabunifu, na kuacha ujanja ujanja maana kutumia kitu hukatazwi lakini uombe kwa muhusika akupe baraka zake", amesema Domo Kaya.
Msanii Domo Kaya.
Hivi karibuni msanii Alikiba ameonesha kutumia msemo huo 'yebaba' katika wimbo wake mpya wa 'Kadogo' aliouachia mwishoni mwa mwaka uliopita na kuupa umaarufu mkubwa kwa mashabiki wake badala ya ule ambao ulizoeleka wa 'Yooo', ambao alikuwa akiutumia hapo kabla.
Bofya link hapo chini kutazama video, Domo Kaya amefunguka zaidi.