Jumatano , 12th Mar , 2014

Staa wa muziki kutoka Nigeria, 2face Idibia naye ameamua kuonyesha uwezo mwingine alionao katika sanaa, ambapo anatarajia kuonekana hivi karibuni katika filamu mpya ambayo inatengenezwa huko Nollywood akiwa kama mwigizaji.

Filamu hii mpya ambayo itamuuzisha sura vilivyo 2Face, imepatiwa jina Make a Move ikiwa inabeba maudhui ya kimuziki, ikiwa na lengo kubwa la kufundisha watazamaji wake juu ya mambo muhimu katika kucheza muziki.

Filamu hii inatarajiwa kutoka tarehe 6 mwezi Juni, na ndani yake imeshirikisha pia mastaa wengine wa filamu kutoka Nigeria, akiwepo Majid Michel, Beverly Naya, Wale Adebayo na Tina Mba.