Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wezi kufukuzwa na kunyang'anywa leseni

Jumanne , 25th Jul , 2017

Naibu Waziri wa Afya, Mh. Hamisi Kigwangalla ameahidi kuwafutia leseni, kuwanyang'anya vyeti na kuwafikisha kwenye mikono ya sheria watumishi wa sekta ya afya wenye tabia ya kuiba dawa na kwenda kuuza sehemu nyingine.

Mh. Kigwangalla ametoa ahadi hiyo leo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Itigi mkoani Singida kwenye ziara ya Rais Magufuli ya kuzindua miradi mbalimbali, ambapo Dkt. Kigwangalla amemshukuru rais kufanya maboresho makubwa katika sekta ya afya na kumuahidi tatizo la kuibiwa dawa hospitalini halitakuwepo tena.

"Wananchi hawatakosa dawa tena pindi watakapokwenda kwenye vituo vya afya vya Umma hapa nchini. Jambo la ukosefu wa dawa lilikugusa sana kipindi cha kampeni nakuahidi dawa ulizotupatia hazitaibiwa tena na niweke wazi kwamba mtumishi atakayethubutu kufanya hivyo nyundo nzito itamuangukia. Ukiachana na kwamba tutamfukuza kazini lakini pia tutamnyang'anya leseni yake pamoja na cheti ili asifanikiwe popote na baada ya hapo tutampeleka kwenye mikono ya sheria ilia ashitakiwe kwa makosa ya jinai kwani uwizi wa dawa ni sawa ni uwizi mwingine," Kigwangalla.

Hata hivyo Mh. Kigwangalla ameongeza kwamba kwa sasa bado wanashughulika na wauguzi wenye kauli chafu dhidi ya wagonjwa ili kuikomesha kabisa tabia hiyo.

"Ili kukomesha kabisa lugha chafu wanazozitoa baadhi ya wahudumu wa afya tumewataka kuweka na rekodi ya kila mzazi aliyepoteza mtoto ili tujue hayo matukio yanasababishwa na nini," aliongeza

Pamoja na hayo Naibu Waziri ameshukuru  Rais Magufuli kuboresha vituo vya afya kama vyumba vya upasuaji ambavyo vitasaidia changamoto zitokanazo na uzazi. 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali