Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waliohusika upotevu vielelezo mahakamani kukiona

Alhamisi , 15th Jul , 2021

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Dkt. Saada Mkuya Salum amezitaka mamlaka husika kuwachukulia hatua wale wote wanaohusika na kupoteza vielelzo vya madawa katika mamlaka zenye dhamana ya madawa ya kulevya.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Dkt. Saada Mkuya Salum

Kauli hiyo imekuja kufuatia kutokuridhishwa na utunzaji wa vielelezo hivyo katika Mahakama na Polisi Kisiwani Pemba jambo ambalo ameeleza kuwa linaweza kuwa ndiyo kikwazo kwa kesi nyingi za madawa kuondoshwa Mahakamani bila ya watuhumiwa kupewa adhabu.

“Kete 4763 za heroin tumetafuta vielelezo hatujaziona lakini hili hatutoliachia hapa kwa sababu tumeona kumekuwa na mapungufu mkubwa sana ya usimamizi kesi nyingi za heroin zimeachiwa lakini hata uhifadhi wa vielelezo hatutaachia hivi hata hao ambao wamehusika kwa namna moja au nyingine kupoteza hivyo vielelezo basi watawajibika katika hili,” amesema Dkt. Saada.

“Lakini kwa hali hii na vielelzo hivi tunapimaje kama huu unga umerudi mtaani hatuna uhakika sisi tunalaumiwa kwamba hatufanyi kazi kumbe uzembe uko kwa watendaji wenu,” amesema Luteni Kanali Burhan Zubeir Nassor Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Kudhibiti Madawa ya Kulevya Zanzibar.

Nayo Kamati ya Uteketezaji Madawa ya Kulevya Zanzibar imesema haijaridhishwa na namna ya utunzaji wa vielelezo vya madawa katika mamlaka zenye dhamana hizo Kisiwani Pemba jambo ambalo linaweza kutoa mwanya kwa madawa hayo yaliyokamatwa kurudi kwa watumiaji mitaani.

Kwa upande wake Mrajisi wa Mahakama Zanzibar Mohamed Ali Mohamed ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo ametaka kamati kuchukua hatua stahiki juu ya mapungufu yaliyojitokeza na Mahakama nayo itachukua hatua kwa wale waliozembea majukumu yao.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali