Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

RC Kunenge atoa maagizo kwa wakazi wa Kunduchi

Jumapili , 22nd Nov , 2020

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Aboubakar Kunenge, amewaelekeza baadhi ya wakazi wa eneo la Kunduchi Mtongani ambao nyumba zao zimepitiwa na ujiuji wa volcano ya tope linalofuka kutoka ardhini kuhama Mara moja ili kujikinga huku Serikali inaendelea kufanya utafiti juu ya athari iliyotokea.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Aboubakar Kunenge

RC Kunenge akiongozana na wajumbe wa kamati ya usalama ya Mkoa, leo, wamefika Katika eneo hilo na kushuhudia uwepo tope linalotoka ardhini na kupanda Katika uso wa ardhi jambo lililosababisha baadhi ya nyumba kutitia, kupasuka nyufa na mifugo kutitia hivyo kuzua taharuki kwa wakazi wa eneo hilo.

             RC Kunenge wa tatu kushoto akiwa katika mmoja ya nyumba iliyopata athari ya 'volcano ya tope'

Kutokana na hali hiyo RC Kunenge amemuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, kuweka alama za hatari Katika eneo hilo wakati Serikali chini ya Taasisi ya Geologia na utafiti wa Madini Tanzania ukiendelea kupitia ukubwa wa eneo lililoathirika.

Pamoja na hayo RC Kunenge amesema Serikali inaangalia utaratibu wa kuwapatia wananchi wa eneo hilo viwanja vingine ili waweze kuendelea na maisha kama awali.

Kwa upande wake Mtafiti kutoka Taasisi ya Geologia na utafiti wa Madini Gabriel Mbogoni amesema matokeo ya awali wamebaini chanzo cha tope hilo ni mgandamizo uliosababishwa na uwiano wa maji na chembechembe za udongo kuharibika na kusababisha tope ambalo linasukumwa kutoka chini kwenda kwenye uso wa ardhi.

Aidha Bwana Mbogoni amesisitiza kuwa tope hilo wamelipima na kukuta likiwa na joto la kawaida hivyo halina uhusiano wowote na ile volcano inayorusha majivu na Moto utokanao na miamba iliyoiva hivyo eneo hilo kwa Sasa ni tete na halifai kwa shughuli za Ujenzi Wala makazi.

HABARI ZAIDI

Mbunge wa Kilosa Profesa Palamagamba Kabudi

"Ndege ijayo ipewe jina la Mwl Nyerere" - Profesa

Baadhi ya Wanachi wa Kata ya Msowero, wakiwa Katika Mkutano wa Hadhara na Mkuu wa Wilaya

Mwenyekiti atiwa mbaroni kwa kuuza mlima, Msowero

Sehemu iliyokumbwa na Mafuriko Kusini mwa Brazil

Wanaokufa kutokana na mafuriko waongezeka Brazil

Baadhi ya Wabunge Wakichangia Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Uchukuzi

Serikali yashauriwa kuwa bunifu sekta ya usafiri

Baadhi ya Wananchi Wakishudia Ajali Iliyomgonga Mwendesha Bodaboda

Watatu wanusurika kifo, scania ikimgonga bodaboda

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Afya, Usalama na Mazingira kutoka GGML, Dk Kiva Mvungi (kushoto) wakimpatia vifaa kinga mmoja wa washiriki wa mafunzo kwa madereva bodaboda wa jiji la Arusha.

Bodaboda 200 Jijini Arusha wanolewa na kufundwa

Rajab Abrahaman Abdalah, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Tanga

CCM Tanga yaijibu CHADEMA kuhusu huduma za kijamii

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama

Wazazi simamieni maadili kwa watoto