Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wizara yatoa agizo kupunguza ukatili katika jamii

Jumapili , 22nd Nov , 2020

Katibu Mkuu, Wizara ya Afya Idara Kuu ya Maendelo ya Jamii, Dkt. John Jingu, amesema ujenzi wa nyumba bora katika jamii utasaidia wananchi kuwa na makazi bora na kuondokana na vitendo vya ukatili ambavyo wakati mwingine huanzia katika ngazi ya familia.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendelo ya Jamii Dkt. John Jingu akionesha Mwongozo ya uboreshaji makazi

Dkt. Jingu ameyasema hayo katka kijiji cha Ilalangulu, kilichopo katika Halmshauri ya Mpwimbwe, mkoani Katavi , wakati akihamasisha Kampeni ya kuboresha Makazi inayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini ambapo amesema, wizara inatekeleza mipango ya maendeleo ambayo imepewa kipaumbele katika Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 ambayo imeweka wazi umuhimu wa makazi bora kwa taifa lenye afya.

“Wizara inahamashisha wananchi kuboresha makazi yao kwa kujiunga katika vikundi ili kupata mikopo itakayowawezesha kuboresha makazi”. amesema Dkt. Jingu 

Ameongeza kuwa na makazi bora ni maendeleo ya jamii kwani makazi bora yanasaidia familia kuwa na Amani na utulivu katika ustawi wao kwa ujumla, “Ukiwa hauna nyumba bora unakaribisha wageni wengine kama mende, kunguni, panya na wadudu hatarishi kagtika makazi wanaoondoa amani katika familia” alisema Dkt. Jingu

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpwimbwe Godfrey Nkuba amesema Halmashauri hiyo imefika asilimia 70 ya makazi bora katika vijiji na Kata zilizopo.

Naye mmoja wa wananchi aliyeboresha makazi yake kwa kutumia kipato chake na mikopo cha vikundi Elizabeth Nyanda amesema kuwa mpango wa Taifa wa kunusuru kaya masikini (TASAF) umemsaidia kupata mtaji wa biashara iliyomuwezesha kujenga nyumba mbili za kisasa na kutoka katika nyumba ya tope na nyasi.

Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii inaendesha Kampeni maalum ya kuhamasisha jamii kuboresha makazi yao ikiwa na kauli mbiu isemayo: “Piga Kazi Boresha Makazi”

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali