Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba
Ametoa Maagizo hayo wakati akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), jijini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine ametoa mwelekeo wa utekelezaji wa Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2021/2022.
“Nataka mkasimaie ugawaji wa rasilimaji fedha kwa kila Wizara ili tukirudi tena bungeni kuelezea utekelezaji wa bajeti kusiwe na mahali ambapo fedha za maendeleo zitakuwa zimepelekwa chini ya asilimia 50” Alisisitiza Dkt. Nchemba.
Aidha, aliwaagiza watumishi hao kujiwekea utaratibu wa kufuatilia kwa umakini utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo inayotokana na fedha zinakazotolewa na Serikali ili kuona utekelezaji wake na kama zimetumika kama ilivyokusudiwa kwa kuwa itasaidia miradi kukamilika kwa wakati.
Aidha, aliwataka watumishi hao kuendelea kufanya kazi kwa weledi mkubwa kwa kuzingatia maadili, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma.
Dkt. Mwigulu aliongeza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Samia Suluhu Hassan anaitegemea wizara katika masuala yote ya uchumi hivyo ni jukumu la Wizara kuhakikisha inatoa ushauri mbalimbali wa kitaalamu kuhusu masuala ya uchumi kwa maendeleo ya nchi.







