Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wizara zilizofanya manunuzi nje ya bajeti zatajwa

Alhamisi , 8th Apr , 2021

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere ameisoma ripoti yake ya mwaka wa fedha 2020/21 mbele ya waandishi wa habari leo Aprili 8, 2021 jijini Dodoma na kubainisha baadhi ya taasisi zikiwemo wizara zilizofanya manunuzi nje ya utaratibu.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere (kushoto)

CAG Kichere amezitaja baadhi ya wizara hizo ambazo zimefanya manunuzi ya bidhaa na huduma nje ya mpango wa manunuzi wa mwaka kuwa ni Wizara ya Afya, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Utalii, Mifugo na Uvuvi pamoja na taasisi nyingine kama Tume ya taifa ya Uchaguzi (NEC).

''Ununuzi uliofanyika nje ya mpango wa mwaka wa manunuzi, jumla ya taasisi 7 ambazo ni TRA, Wizara ya Afya, Zimamoto, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Manispaa ya Morogoro, Wizara ya mambo ya Nje, Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilifanya ununuzi wa vifaa na huduma wa zaidi ya shilingi Bil 15.129,'' ameeleza CAG Charles Kichere.

Mbali na ripoti katika eneo hilo la manunuzi, CAG pia amezitaja Halmashauri, Manispaa pamoja na Taasisi ambazo zimepewa hati mbaya.

''Mwaka huu nimetoa hati mbaya kwa Halmashauri za Wilaya Shinyanga, Singida, Itigi na Igunga, Wilaya ya Sikonge, Urambo, Momba, Manispaa ya Tabora, Hospitali ya Rufaa Morogoro, Tume ya UNESCO,” amesema CAG Charles Kichere.

Ikumbukwe kuwa Machi 28, 2021 CAG Charles Kichere aliisoma ripoti hiyo na kuiwasilisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi