Jumamosi , 31st Aug , 2019

Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu ametoa tahadhari ya Ugonjwa wa Ebola kwa Wananchi katika mikoa yote ya Tanzania.

Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu

Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Afya, imetoa elimu kwa watanzania juu ya namna ya kuepuka ugonjwa huo ambao ni hatari.

Waziri Ummy amewataka wananchi kuchukua hatua stahiki za kujikinga na kudhibiti ugonjwa huu usiingie nchini.

Ebola imekuwa tishio kwa nchi kadhaa zinazopakana na Tanzania ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
 

Tazama Video hapo chini ikieleza namna ya kujinga au kujua dalili za Ebola.