Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
Msaada huo umekabidhiwa na Katibu wake Tommy Malenga, kwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela na kusema mbali na msaada wa TV hizo, pia vimetolewa vifaa kinga zikiwemo ndoo 270 za kunawia mikono kwa lengo la kuchochea ari ya wananchi kunawa mikono mara kwa mara.
"Tunataka na wananchi wetu walioko vijijini wanapata fursa ya kuangalia TV, hivyo tunakabidhi TV 40 na zitafungwa katika kila Kijiji kilichopo katika Jimbo la Isimani" amesema Katibu huyo.
