Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wazawa 7,713 waajiriwa bwawa la Nyerere

Jumapili , 17th Oct , 2021

Katika kuendelea kuhakikisha wananchi wanapata ajira za kudumu za zile za muda mfupi ili kujipatia kipato, serikali imeweka wazi kuwa kipaumbele cha ajira katika miradi ya ndani ni kwa wazawa wenye sifa.

Sehemu ya mradi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere

Hayo yameelezwa na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa wakati akitoa taarifa ya wiki, ambapo amesema katika mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere asilimia 89 ya wafanyakazi ni watanzania.

''Mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere una Wafanyakazi Watanzania 7,713 sawa na 89% ya wafanyakazi wote 8,635. Mpaka sasa Wakandarasi wameshalipwa Sh Trilioni 2.832 kati ya Trilioni 6. 558 zitakazotumika kugharamia ujenzi huu,”amesema Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa.

Kwa upande mwingine amesema serikali inaendelea kuifungua nchi kwa kuhakikisha barabara zote zinapitika na kuwawezesha watu kufanya shughuli zao za kijamii na kiuchumi bila changamoto hata kama wapo vijijini iwe rahisi kufikia huduma maeneo ya mijini.

''Hadi Juni, 2021, TARURA imetumia Sh Trilioni 1. 297 kutengeneza KM 24,979 za barabara, KM 955.35 kwa kiwango cha lami, KM 16,857 kwa kiwango cha changarawe pia wamejenga madaraja 231 na makalvati mapya 1,325. Mwaka huu wa fedha, Serikali imeitengea TARURA Bilioni 934,” ameongeza Gerson Msigwa, Msemaji Mkuu wa Serikali.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi