Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watano wafa ajalini Simiyu

Ijumaa , 1st Jul , 2022

Watu watano wamefariki Dunia na wengine watano wamejeruhiwa katika ajali ya gari dogo, iliyotokea eneo la Lugulu Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Somanda Mjini Bariadi, Dk. Emmanuel Costantine, amesema katika majeruhi hao mmoja ni mtoto mwenye umri wa miaka miwili.

Tukio hilo la kusikitisha limehusisha gari dogo maarufu kwa jina la mchomoko T 789 DKM, lililokuwa limebeba abiria likitoka Wilaya ya Maswa kwenda Mjini Bariadi mkoani hapa

Dk. Emmanuel amesema katika majeruhi hao watano, wanne ni wa kiume na mmoja ni wa kike na miongoni mwa hao wa kiume mmoja ni mtoto wa miaka miwili. 

Amesema  hali ya majeruhi saizi (sasa hivi) inaendelea vizuri, miongoni mwao watatu walipata mshtuko wa ubongo lakini tayari wamezinduka na hali zao zinaendelea kuimarika

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu, Blasius Chatanda, amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa gari hilo, lililopinduka baada ya kugonga nguzo ya barabarani, wakati dereva wa gari hilo Seleman Masele (26) akimkwepa mwenda kwa miguu.

Kamanda Chatanda alipoulizwa na EATV iwapo dereva huyo wamemfanyia vipimo kujua endapo alikuwa ameelemewa na kilevi au mserereko wa dawa za kulevya, amesema bado hajafanyiwa vipimo kujua mambo hayo, hivyo hawezi kusema ndiyo au hapana.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali