Jaji Joseph Sinde Warioba
kwa makaburu.
Akizungumza na EATV&EA Radio Digital leo Septemba 8, 2019, Jaji Warioba amesema kuwa licha ya wengi kuiona Zimbabwe haiko sawa kwa kipindi hiki, lakini ni kiongozi pekee aliyeitoa Zimbabwe katika wakati mgumu wa masuala ya ubaguzi wa waafrika kutothaminiwa na kuweka usawa wa kibinadamu.
''Ni kweli sasa hivi Zimbabwe ina matatizo lakini siyo peke yake yanatokea, Mugabe kama kiongozi pamoja na yote yaliyotokea hakuna atakayebisha kwamba alikuwa ni mmojawapo wa viongozi imara waliojua kupigania haki, na alipopata uongozi alijitahidi kuifanya Zimbabwe iwe mahali ambapo watu wote wanaishi sawa'' amesema Jaji Warioba.
Akizungumzia masuala ya ardhi ya Zimbabwe Jaji Warioba amesema, wazungu wengi walipora ardhi kubwa na yenye rutuba na kuwaachia wazawa maeneo madogo na hiyo ndiyo imekuwa chanzo cha matatizo ya sasa na kuomba suala hilo lipatiwe ufumbuzi kwa kuaminini kwamba Zimbabwe itatulia.

