Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanasiasa wawatibua wananchi

Jumatano , 13th Dec , 2017

Wimbi la kuhama vyama kwa wanasiasa nchini limewachanganya wananchi kiasi cha kushindwa kutambua Chama kipi kinafaa ama kiongozi gani mwenye msimamo kisiasa.

''Siasa imekuwa na mihemko kwa kipindi hiki vuguvugu linaendelea, hii inasababisha sisi kutoelewa kuwa upinzani au chama tawala yupi yupo sahihi, maana yule aliyekataliwa CCM siku hizi anakubalika upinzani na aliye kataliwa upinzani anakubalika Chama tawala'', amesema mfanyabiashara wa bidhaa ndogondogo Kelvin John Mjema.

Hayo yamebainishwa na wananchi tofauti katika soko la Mwenge wakati wakizungumza na East Africa Television.
Naye Aisha Ramadhani Mama Ntilie katika eneo la Mwenge amefunguka na kusema yeye kwasasa vyama vimemtibua na hataki kabisa kushabikia chama chochote.

"Sihitaji kushabikia mtu kwasasa, maana unashabikia mtu na chama fulani ghafla siku mbili unamuona kaondoka kaenda chama kingine, na wewe unahama, ukifika huko baada ya muda naye anahama sasa unashindwa kufahamu ufanye nini, kwakweli CUF, CCM na CHADEMA wanatuchanganya sana kwasasa", amesema Aisha.

Kumekuwa na wimbi kubwa la viongozi wa siasa kuhama vyama vyao huku wakisababisha majimbo waliyoyaacha wazi kuandaliwa uchaguzi na NEC ambao hugharimu zaidi ya  shilingi milioni 80.

Miongoni mwa majina makubwa ambayo  yamehama vyama siku za hivi karibuni ni pamoja na aliyekuwa Mbunge  wa Singida Kaskazini Lazaro Nyalandu kuhamia CHADEMA aliyekuwa Mbunge wa Kinondoni kupitia CUF Maulid  Mtulia kuhamia CCM pamoja na makada wengine mbalimbali. 
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali