Jumanne , 12th Jul , 2022

Mganga Mkuu Mkoa wa Mtwara, Hamad Nyembea amewataka wananchi mkoani humo kutokuwa na hofu juu ya uwepo wa ugonjwa wa kutokwa na damu puani, ugonjwa ambao umeripotiwa katika mkoa wa Lindi, amesema ugonjwa huo ni wa kuridhi, na unachangiwa pia na hali ya hewa 

Aidha kuhusu kuwapo kwa ugonjwa huo Mkoani Mtwara Nyembea anasema,  mpaka sasa hakuna taarifa ya uwapo wa ugonjwa huo Mkoani humo,

Nyembea ametoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Mtwara, kufika haraka katika kituo cha afya  pindi watakapoona dalili yoyote ya kutokwa na damu puani