Mke wa Waziri Mkuu , Mama Mary Majaliwa akizungumza na wanafunzi wa sekondari ya Vwawa.
Nasaha hizo zimetolewa na mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa alipokuwa akizungumza na na wanafunzi wa shule ya Sekondari Vwawa wilayani Mbozi.
“Nawasihi mtumie muda huu kusoma kwa bidii ili muweke msingi imara kwa ajili ya kujenga maisha yenu ya baadae. Msikatishe masomo yenu. Utumieni muda huu vizuri ili msije mkaujutia baadae, kwani wakati ni mali ukipita umepita,” Mama Majaliwa.
Alisema ni vizuri wakasoma hadi chuo kikuu na kwamba wasikimbilie kufanya mambo yasiyowahusu kwa sasa kwani mshika mawili moja lazima limponyoke.
Waziri Mkuu Majaliwa akiwa na mke wake mama Mary Majaliwa (Picha na maktaba).
Mke wa Waziri Mkuu alisema wanafunzi hao wakisoma hadi elimu ya juu watakuwa na uwezo wa kutambua jambo lipi ni jema na lipi ni baya.
“Kilichonifurahisha zaidi ni kwa sababu mimi pia ni mwalimu kwa hiyo ninavyoona wanafunzi wako vizuri kama hivi nafurahi sana, hivyo nawaomba msome kwa bidii,” aliongeza
Pamoja na hayo serikali imetunga sheria kali dhidi ya watu wanaosababisha watoto wa kike kukatisha masomo yao kwa kuwapa mimba au kuwaoa.
Mke wa Waziri Mkuu aliambatana na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika ziara ya mkoa Songwe.