Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wanafunzi wa awali wanasoma kama chuo Kikuu

Ijumaa , 16th Apr , 2021

Mdau wa Elimu nchini Richard Mabala amesema kuna haja ya Serikali kupitia Wizara ya Elimu na idara zake mbalimbali kupitia upya mifumo ya elimu na ufundishaji ili kuiboresha kwa manufaa ya wanafunzi wanaopita kwenye mifumo hiyo.

Mdau wa Elimu nchini Richard Mabala

Mabala ameyaeleza hayo leo kwenye mahojiano na kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, ambapo ametolea mfano namna wanafunzi wa shule za awali na msingi wanavyolazimika kutumia muda mwingi zaidi darasani kuliko uhalisia wa mahitaji ya elimu yao.

''Tukianza kwenye shule za awali wanasoma kama wanafunzi wa chuo kikuu, wanakaa kwenye madawati siku nzima. Mtoto mdogo anatakiwa kucheza kupanua ubunifu wake na uwezo wa kuchambua mambo,'' amesema Richard Mabala.

Aidha amesema mfumo wa sasa unamnyima mwanafunzi wigo mpana wa kuwa mbunifu ndio maana wahitimu wengi hata wale wa elimu ya juu wanashindwa kujiari.

''Tukiangalia kwa sasa kwenye mfumo wetu wa elimu, ubunifu unafundishwa wapi katika elimu yetu? Kwahiyo ni lazima tuangalie upya ili kuboresha uwezo wa wahitimu wetu,'' ameeleza.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali