Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Walimu waandamana Kasulu, Kigoma

Jumamosi , 6th Dec , 2014

Walimu zaidi ya 200 katika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wameandamana na kumpa wakati mgumu mkurugenzi wa halmashauri ya Kasulu Masalu Mayaya, wakishinikiza kulipwa kwa madai yao mbalimbali yanayofikia zaidi ya shilingi milioni 172.

Walimu zaidi ya 200 katika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wameandamana na kumpa wakati mgumu mkurugenzi wa halmashauri ya Kasulu Masalu Mayaya, wakishinikiza kulipwa kwa madai yao mbalimbali yanayofikia zaidi ya shilingi milioni 172.

Viongozi wa chama cha walimu pamoja na walimu hao kutoka shule mbalimbali za sekondari na msingi wamesema kwa muda mrefu wanaidai serikali fedha za likizo, uhamisho, mapunjo ya mishahara, matibabu na hawapandishwi madaraja kwa mujibu wa sheria.

Walimu hao pia wamemshutumu Afisa Elimu wa halmashauri hiyo Kalugutu Zuberi kuwa amekuwa kikwazo kwa maendeleo ya elimu katika wilaya hiyo na kwamba licha ya serikali kukataza uhamisho wa watumishi bila malipo halmashauri hiyo imekuwa ikihamisha walimu bila ya kuwalipa.

Mkurugenzi wa halmashauri ya Kasulu Masalu Mayaya akizungumza na walimu hao, ameahidi ofisi yake kushughulikia matatizo hayo kwa haraka na kwamba tatizo la kuchelewa kwa malipo linatokana na uhakiki wa viambatanisho na fedha kutoka serikalini.

Katika kikao hicho cha pamoja kati ya mkurugenzi wa Kasulu na walimu, wamekubaliana kupitia upya madai kwa muda wa wiki moja na kuanza kutoa barua za kupanda madaraja mwezi ujao.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi