Jumanne , 6th Jun , 2023

Wafanyabiashara wa nyanya za rejareja katika soko la Temeke Stereo Jijini Dar es salaam wamelalamikia kitendo cha wafanyabiashara wa nyanya za jumla kuipandisha bei ya nyanya kutoka shilingi elfu 25 mpaka elfu 30 kwa Tenga hadi kufikia shilingi elfu 50 mpaka 55 kwa Tenga

Wakizungumza na #EATV wafanyabiashara hao waliofika sokoni hapo leo wamesema kitendo hicho kimesababisha kuwakwamisha kufanya biashara hiyo kutokana na kutotarajia kupanda ghafla kwa bei ya nyanya katika soko hilo

Nao wafanyabiashara wa nyanya za jumla katika soko hilo la Temeke Stereo wamesema kupanda kwa bei ya nyanya kumetokana na mvua zinazoendelea kunyesha maeneo ya vijijini zinakotoka nyanya hizo

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kitengo cha nyanya katika soko hilo Banzi Kaunda amesema hiyo ni hali ya kawaida kutokea jambo ambalo wafanyabiashara hao wa nyanya za rejareja wanapaswa kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki