Alhamisi , 17th Jul , 2025

Israel imeongeza operesheni zake za kijeshi nchini Syria, ikishambulia eneo la kuingilia makao makuu ya Wizara ya ulinzi mjini Damascus, pamoja na jeshi.

Shambulizi la Israel nchini Syria hivi karibuni ni la siku ya tatu mfululizo, wakati ambapo ghasia zikiendelea kuongezeka kati ya vikosi vya serikali na wapiganaji wa Druze kwenye mji wa kusini wa Sweida.

Vyanzo vya usalama vya serikali ya Syria vimethibitisha kuwa droni zipatazo mbili zimeshambulia jengo la wizara, huku ikiripotiwa kuwa maafisa wametafuta hifadhi katika handaki. Televisheni ya serikali ya Elekhbariya, imeripoti kuwa raia wawili wamejeruhiwa.

Taarifa nyingine zinaeleza kuwa Israel imefanya shambulizi la anga karibu na makaazi ya rais mjini Damascus.

Jeshi la Israel limesema linafuatilia kwa karibu hali inayoendelea, hasa hatua zinazochukuliwa dhidi ya raia wa jamii ya Druze kusini mwa Syria. Awali, Waziri wa zamani wa Ulinzi wa Israel, Yoav Gallant, alionya kuwa Israel haitowaacha watu wa jamii ya Druze na inaweza kuzidisha mashambulizi hadi vikosi vya Syria vitakapoondoka kwenye eneo hilo.