Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wachimbaji wadogo walia na Rais Magufuli

Jumanne , 28th Mar , 2017

Baadhi ya wachimbaji wadogo ambao wanadai kuwa ni sehemu ya wamiliki wa makontena yaliyozuiliwa katika bandari ya Dar es Salaam yakiwa na shehena ya mchanga wa madini, wameiomba serikali kupitia upya zuio hilo kwa maelezo kuwa limeathiri biashara.

Wachimbaji wadogo wadogo wanaosafirisha nje ya nchi mchanga wenye masalia ya madini wakizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam hii leo

Wakizungumza katika mkutano na wanahabari leo Jijini Dar es Salaam, wachimbaji hao wamesema kimsingi hawapingani na uamuzi huo wa serikali bali wanaunga mkono kwani uamuzi huo unaotokana na agizo la Rais John Pombe Magufuli alilolitoa takribani mwezi mmoja uliopita, linayalenga makampuni makubwa na siyo wao ambao ni wamachinga kwenye sekta ya madini.

Wamesema tangu lilipotolewa agizo la kutosafirisha nje mchanga wenye masalia ya madini, wamekuwa wakipata hasara kubwa ambapo mmoja wa wachimbaji hao amesema anaingia hasara ya zaidi ya shilingi milioni nne kwa siku kutokana na kusitisha shughuli za uchimbaji huku akitakiwa kulipia wastani wa dola ishirini kama gharama ya utunzaji kwa kila kontena linaloshikiliwa pale bandarini.

Sehemu ya makontena ya mchanga yanayoshikiliwa bandarini

Kwa mujibu wa maelezo ya wachimbaji hao akiwemo Bw. Mohammed Mkwayu anayemiliki kampuni ya Kambi Mineral Resources inayofanya shughuli zake wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma na Bw. King Selemani anayemiliki kampuni ya Wit Mining inayofanya shughuli zake wilaya za Kongwa na Mpwapwa; zaidi ya kontena sitini za wachimbaji wadogo wadogo zimezuiliwa zisisafirishwe kwenda nje ya nchi na kwamba hatua hiyo imechukuliwa huku wakiwa na vibali vyote vinavyowaruhusu kufanya biashara hiyo.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu