![](http://eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2024/03/23/water.jpg?itok=6Clyt7O6×tamp=1711197906)
Chanzo cha Maji ya Kisima
Wakizungumza na EATV baadhi ya wananchi wameleza kuwa changamoto hiyo ambayo imedumu kwa miaka kadhaa sasa inakwenda kuondoka na wao kunusuru ndoa zao, kuondokana na athari za vifo vilivyotokana na maradhi ya mlipuko baada ya kutumia maji ya visima ambayo si safi na salama.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga wakati akifungua mradi wa maji wenye gharama ya zaidi ya TZS. milioni 290 uliowezeshwa na shirika la World Vission ameielekeza mamlaka ya RUWASA mkoani humo kuhakikisha zoezi la usambazaji wa maji kupitia mradi huo linakuwa na gharama nafuu kwa wananchi.
Kwa upande wake Meneja wa Shirika la World Vission Kanda ya Kaskazini anaeleza kuwa mradi huo umesaidia kupunguza mwendo wa zaidi ya saa moja kwa wananchi kuyafuata maji na sasa wakiyapata maji hayo kwa dakika tano mpaka kumi.