Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ujumbe wa Waziri Mkuu Siku ya Eid

Ijumaa , 14th Mei , 2021

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa leo Mei 14, 2021 ameshiriki swala ya Eid iliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam, na kuwasihi waumini wa dini ya Kiislamu kuhudhuria katika Baraza la Eid litalofanyika katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa

Akizungumza katika Swala hiyo Waziri Mkuu amewasihi Waislamu kujitokeza kwa wingi katika Baraza hilo ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, atakuwa mgeni rasmi.

“Niwasihi Waislamu wenzangu wote, tuhudhurie kwenye Baraza la Eid, mnatambua Rais wetu anakuja kwenye Baraza la Eid kwa mara kwanza ni vyema tukajitokeza kwa wingi kuja kupata neno kwa kiongozi wetu wa nchi,” amesema Mhe. Majaliwa.

Awali Mhe. Majaliwa amesema hawana budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwalinda hadi kufikia siku ya Eid, huku akisema kuwa ujumbe mahususi wa siku ya Eid utataolewa rasmi alasiri na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kufunga siku zote 30 na hatimaye leo tumeamka salama ni jambo la kumshukuru, tunatambua tutaendelea na siku 6, na mimi niwatakie kila kheri katika Sikukuu hii, huo ndio ujumbe wangu kwa leo," amesema Waziri Mkuu.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu