Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uhuru mgeni rasmi maadhimisho ya uhuru Tanzania

Jumanne , 4th Mei , 2021

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa mualiko rasmi kwa Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanzania  yatakayofanyika mwezi Desemba mwaka huu.

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta.

Rais Samia ametoa mualiko huu rasmi wakati akihitimisha hotuba yake mbele ya viongozi na  waandishi habari nchini Kenya, akiwa katika ziara yake aliyoanza leo nchini humo ambapo ameahidi kuwa Tanzania itakuja kwa kasi kuwekeza nchini Kenya ili kukuza ujazo wa biashara.

Awali Rais Samia amesema nchi za Kenya na Tanzania zimekubaliana kushughulikia vikwazo vilivyopo hususan visivyo vya kodi katika mipaka ya nchi hizo mbili ili  kukuza biashara na uwekezaji baina ya nchi hizo.

“Kwa lengo la kukuza biashara na uwekezaji kati yetu tumekubaliana kuendelea kushughulikia baadhi ya changamoto hususan  vikwazo visivyo vya kodi ambavyo vinatokea katika mipaka yetu, Tumekubaliana kuwa Mawaziri wetu wa Afya kukaa na kuangalia namna ya kurahisisha mfumo wa kuingia na kupimwa haraka watu wetu kwenye mipaka katika masuala haya yaliyoingia ya Covid 19, ili waweze kupita na biashara ziendelee'',” amesema Rais Samia

Naye Rais Uhuru Kenyatta ameeleza kufurahishwa na ujio wa Rais Samia huku akisema makubaliano yao katika kuimarisha mahusiano baina ya nchi hizo mbili yatasaidia kukuza  na kutanua wigo wa biashara.

“Mawaziri wetu wameambiwa wahakikishe wanakutana mara kwa mara ili kuzingatia uhusiano wetu na kutatua shida ndogondogo miongoni mwa wananchi, suala la mahusiano tutaendelea kuyaimarisha kutoka safari za ndege, za reli na za kupitia baharini, kule upande wa kanda ya ziwa,” amesema Rais Uhuru Kenyatta

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA