Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Ugonjwa wa ajabu waibuka Mbeya wauwa 15

Jumamosi , 6th Feb , 2021

Wananchi wa kata ya Ifumbo wilayani Chunya mkoani Mbeya, wameripotiwa kuugua ugonjwa usiofahamika ambao mtu akiugua anatapika damu mpaka anapoteza maisha, na mpaka sasa tayari watu zaidi ya 15 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 50 wanaendelea kuugua.

Diwani wa Kata ya Ifumbo, Weston Mpyila

Taarifa ya kuwepo kwa ugonjwa huo usiofahamika imeibuliwa na Diwani wa Kata ya Ifumbo, Weston Mpyila, mbele ya kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Chunya huku akiomba msaada wa kuwanusuru wananchi wake.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya chunya, Ramadhan Shumbi, ameeleza hatua ambazo zimeshachukuliwa na halmashauri yake kukabiliana na ugonjwa huo huku wakiomba kuomba msaada wa kitaalam katika ngazi za juu ili kuubaini na hatimaye kupata tiba yake.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya, Dk. Felister Kisandu, amethibitisha kuwepo kwa ugonjwa huo ambao wameshindwa kuutambua na kudai kuwa ofisi yake imeomba msaada katika ngazi za juu ili wasaidiwe kuutambua na kukabiliana nao.

HABARI ZAIDI

Rose Senyagwa, Mchambuzi wa Masuala ya Hali ya Hewa kutoka TMA

Kimbunga "IALY" kinazidi kusogea Pwani ya bahari

Picha ya Diddy na Cassie enzi za mahusiano yake

Diddy aomba msamaha kumshambulia EX wake Cassie

Rais wa Iran Ebrahim Raisi

Rais wa Iran afariki kwa ajali ya Helikopta

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba,

China yaahidi kuendelea kufadhili miradi Tanzania

Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania, Deodatus Balile

Balile achaguliwa kuwa Mwenyekiti EAES

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu