Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uchunguzi miili iliyokutwa kwenye viroba - Masauni

Alhamisi , 18th Aug , 2022

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamadi Masauni ameagiza kufanywa uchunguzi wa kina ili kubaini mauaji ya kinyama dhidi ya watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni wachimbaji wa madini ambao miili yao ilikutwa kwenye viroba na kutupwa kwenye kijiji cha Lusane kata ya Tunguli Mkoani Tanga

Watu hao wamekutwa wakiwa na majeraha mbalimbali yanayosadikiwa yalitokana na kupigwa na nondo huku shingo zao zikiwa zimevunjwa

Waziri Masauni ametoa agizo hilo wakati alipofanya ziara wilayani humo katika hospitali ya Teule mahali ambapo miili ya watu hao imehifadhiwa, ziara aliyoifanya akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo. 

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba amesema  tukio hilo limeuchafua Mkoa wa Tanga huku akisema vyombo vya dola vitashirikiana kuwabaini wahusika wa tukio hilo. 

Viongozi mbalimbali walioshiriki kwenye ziara hiyo akiwemo Mbunge wa jimbo hilo Omari Kigua, Mkuu wa Wilaya hiyo Abel Busalama, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Tanga, Safia Jongo wamelaani tukio hilo.

Miili hiyo bado haijafahamika licha ya picha zao kuoneshwa kwenye machimbo mbalimbali ya madini katika wilaya ya Kilindi, kwa lengo la kubaini  ndugu na jamaa wa karibu wa watu hao
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi