Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Uchaguzi Mkuu, anguko kwa wapinzani

Alhamisi , 31st Dec , 2020

Oktoba 28, 2020, Tanzania iliingia kwenye joto la uchaguzi, kwa wananchi wake kuwachagua viongozi wao wanaowataka kwa nafasi za kiti cha urais, ubunge, udiwani na wawakilishi kwa upande wa Zanzibar, ambapo kwa mujibu wa viongozi wa serikali walisema kuwa uchaguzi huo ulifanyiaka kwa amani.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe.

Mara baada ya zoezi kukamilika saa 10:00 jioni, zoezi la uhesabuji wa kura ukaanza na baada ya kila jimbo kukamilisha kuhesabu kura lilitangaza washindi wa kiti cha ubunge, na matokeo ya mshindi wa ubunge ya kwanza kabisa kutangazwa yalikuwa ni yale ya jimbo la Hai mkoani Kilimanjaro.

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, alimtangaza mshindi katika kinyang'anyiro hicho kuwa ni Saasisha Mafue wa Chama cha Mapinduzi (CCM), na kumuangusha aliyekuwa mbunge wa muda mrefu wa jimbo hilo kupitia CHADEMA Freeman Mbowe.

Kuangushwa kwa Mbowe katika kinyang'anyiro, kilileta minong'ono mingi kwa wananchi na wapenzi wa chama hicho, huku wengine wakidai kuwa kuangushwa kwake, huenda ikawa ni anguko kwa wabunge wote wa vyama vya upinzani, jambo ambalo lilileta uhalisia mkubwa kwani matokeo yote yaliyofuata yalionesha kuwa CCM ndiyo wanaoongoza.

Kama misemo ya waswahili isemavyo hohehahe hakosi siku yake, ndivyo ilivyotokea kwa chama kikuu cha upinzania nchini Tanzania cha CHADEMA, kwani kiliambulia walau kiti kimoja cha mshindi wa ubunge kupitia chama hicho ambaye ni Aida Khenani, kutoka jimbo la Nkasi Kaskazini.

Katika upande wa matokeo ya urais, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), ilimtangaza pia Dkt. John Magufuli wa CCM, kuwa ndiye mshindi wa kiti hicho, akimshinda mpinzani wake kupitia CHADEMA Tundu Lissu.

Anguko katika uchaguzi mkuu, halikuwa kwa CHADEMA tu bali kwa vyama vingine kama ACT Wazalendo, NCCR-Mageuzi na CUF ambao nao waliambulia kiti kimoja cha ubunge.

 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi