Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tulijua Rais atafanya haya – Kangi Lugola

Alhamisi , 19th Oct , 2017

Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mheshimiwa Kangi Lugola, amesema kasi ya kupambana na rushwa anayoenda nayo Rais Magufuli kwenye uongozi wake, wana CCM walijua atafanya hivyo kutokana na weledi wake.

Kangi Lugola ameyasema hayo leo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha East Africa Breakfast kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba awamu zilizopita kulikuwa na mambo magumu ambayo yalishindikana kutatuliwa ikiwemo vitendo ya rushwa.

Pia Kangi amesema hata alipoingia madarakani Rais Magufuli watu hawakuwa na imani naye wakiamini ni kama wale waliopita, lakini imekuwa kinyume chake kwani sasa serikali haijahofia nguvu ya pesa ya watu hao, na kulifanyia kazi suala la rushwa bila uwoga.

“Yako mambo ambayo walikuwa wanadhani kwamba Rais Magufuli ni rais wa CCM kwa hiyo ni wale wale, lakini sisi tuliokuwa tunamjua kwamba tumepata chombo alipoingia madarakani, tulijua yale mambo magumu ambayo watu walikuwa wanatumia nguvu ya fedha, rushwa zilikuwa zimeshamiri hayawezekani, lakini rais wetu mambo yale magumu ameyafanyia kazi anasonga mbele na hakuna anachoogopa, ili mradi anayafanya kwa mujibu wa katiba”, amesema Kangi Lugola.

Kufuatia hayo Kangi Lugola ametangaza hali ya hatari kwa watu wanaotumia pesa kuvunja sheria ikiwemo kujenga viwanda maeneo ambayo hayaruhusiwi, kitendo ambacho kinachangia uharibifu wa mazingira.

 

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu