
Félix Tshisekedi
Uchaguzi wa Desemba 20, 2023, wa DRC ulikumbwa na changamoto nyingi huku wagombea kadhaa wa upinzani walikuwa wakitaka yafanyike marudio ya uchaguzi huo.
Takribani theluthi mbili ya vituo vya kupigia kura vilichelewa kufunguliwa, wakati asilimia 30 ya mashine za kupigia kura hazikufanya kazi siku ya kwanza ya upigaji kura, kwa mujibu wa waangalizi wa uchaguzi.
Tshisekedi alikuwa akichuana na wapinzani wake kina Moise Katumbi, Martin Fayulu na Denis Mukwege katika uchaguzi ulioghubikwa na malalamiko ya wapinzani hao.