Jumanne , 26th Jul , 2016

Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania(TPSF), kwa kushirikiana na mfuko wa kuendeleza Sekta ya Fedha Tanzania(FSDT),itaendesha mafunzo maalumu kwa wajasiriamali nchini kuhusu namna ya kunufaika na tovuti mpya ya habari kwa wajasiriamali.

Mkurugenzi Mkuu wa TPSF, Godfrey Sembeye

Mkurugenzi Mkuu wa TPSF, Godfrey Sembeye amesema hayo jijini Dar es Salaam, na kueleza kuwa taasisi hiyo imeanzisha vipindi vya redio katika vituo mbalimbali nchini ikiwemo mikoa ya Dodoma, Geita, Kigoma pamoja na Mbeya.

Simbeye amesema vipindi hivyo vitaenda sambamba na warsha za mafunzo zitakazowahusisha wajasiriamali na wadau mbalimbali katika mikoa hiyo.

Ameongeza kuwa tovuti hiyo imelenga kuongeza uelewa wajasiriamali juu ya kukuza biashara, Upatikanaji wa mitaji, mbinu sahihi za kuendesha biashara pamoja namna ya kukuza bidhaa katika masoko.