
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA, hali hiyo inatokana na kuimarika zaidi kwa ukanda wa mvua ambao umeambatana na ongezeko la unyevunyevu katika eneo la bahari ya Hindi.
Maeneo ambayo yataathirika zaidi na mvua hizo ni pamoja na Visiwa vya Unguja na Pemba, mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga, na pia kuna uwezekano wa kusambaa katika mikoa ya Lindi, Mtwara na Morogoro.
TMA imetoa tahadhari kwa wakazi wa maeneo hatarishi, watumiaji wa Bahari pamoja na mamlaka zinazohusika na maafa, kuchukua tahadhari stahiki.