Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TCRA yaonya kuhusu matumizi mabaya ya mitandao

Jumatatu , 8th Sep , 2014

Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania TCRA imeonya kuwa itawachukulia hatua kali baadhi ya watu wanaotumia vibaya huduma za mawasiliano ya simu na mtandao wa intaneti, hasa wale wanaodhalilisha pamoja na kuhatarisha amani.

Msemaji wa Mamlaka ya Mawasiliano TCRA Bw. Innocent Mungy.

Mkurugenzi wa idara ya mawasiliano na elimu kwa umma wa TCRA Bw. Innocent Mungy, ametoa onyo hilo leo kufuatia kile alichosema kuwa ni kuongezeka kwa matukio ya watu kuvunja sheria kiasi cha kuhatarisha amani katika jamii.

Kwa mujibu wa Mungy, watu hao wachache wasio na maadili, wametumia vibaya maendeleo chanya ya upatikanaji wa huduma za mawasiliano nchini, kwa kuweka picha zinazodhalilisha wenzao na zisizoendana na maadili ya Kitanzania.

Msemaji huyo wa TCRA amefafanua kuwa wasichana na mabinti wenye umri chini ya miaka 24 ndio wahanga wakubwa wa udhalilishaji katika mitandao ya kijamii kutokana na wengi wao kupigwa picha za utupu na kuwekwa katika mitandao ilhali wanaume wakiwa sio waathirika wakubwa.

Mungy ametahadharisha kuwa kuna uwezekano wa kutokea matukio ya uvunjifu wa amani katika jamii hasa baada ya kuibuka pia kwa makundi na kambi hasimu zinazogombana kupitia mitandao hiyo.

Amefafanua kuwa sheria ya mawasiliano ya simu na posta ya mwaka 2010 (EPOCA) inakataza watu kutumia vibaya huduma za mawasiliano na ambapo ametaja moja ya adhabu kwa wanaofanya hivyo kuwa ni kifungo cha miezi miezi mitatu jela na faini ya fedha za Tanzania shilingi laki Tano au adhabu zote kwa pamoja.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu