Jumatano , 16th Apr , 2014

Tanzania imetajwa kuwa moja ya nchi kumi duniani zenye kiwango kikubwa cha vifo vya akina mama wajawazito wanaofariki kutokana na matatizo ya uzazi.

Waziri wa afya na ustawi wa jamii nchini Tanzania, Dkt Seif Rashid

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na mkuu wa mradi wa kuzuia vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga ujulikanao kama MAISHA Dakta Dunstan Bishanga.

Akizungumzia tatizo hilo makamu wa rais wa Tanzania Dakta Mohamed
Gharib Bilal amesema Serikali imejizatiti kupunguza vifo hivyo kama
iliyofanya kwa watoto wachanga.