Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TAKUKURU yabaini wizi mpya wa dawa MOI

Jumatano , 13th Jan , 2021

Watumishi 23 wa Kitengo cha Famasia cha Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI), wanachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), kwa tuhuma za kuandika taarifa za uongo katika mfumo wa utunzaji taarifa za kumbukumbu za utoaji dawa na vifaa tiba,

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU,  Brigedia Jenerali John Mbungo.

na kusababisha upotevu wa dawa zenye thamani ya shilingi bilioni 1.2.

Taarifa hiyo imetolewa leo Januari, 13, 2021 na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU,  Brigedia Jenerali John Mbungo, wakati anazungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa watumishi hao wanadaiwa kufanya udanganyifu huo kati ya mwaka 2018 hadi 2020.

Akielezea namna ubadhirifu huo ulivyofanyika, Brigedia Mbungo amesema watuhumiwa hao walikuwa wanaandika taarifa za uongo katika mfumo huo, kwa kuweka idadi kubwa ya vifaa vilivyotolewa tofauti na idadi halisi iliyotolewa kwa wateja na madaktari.

"TAKUKURU kwa kushirikiana na MOI imedhibiti uchepushaji na ubadhirifu wa madawa ya zaidi ya Tsh Bil. 1.2, ambazo zilihujumiwa kwa manufaa binafsi na watumishi wa kitengo cha famasia katika taasisi hiyo"amesema Brigedia Mbungo.

Brigedia Mbungo  ameongeza kuwa, "Ubadhirifu huu umebainika kutokana na uwepo wa tofauti kati ya taarifa za dawa zilizoingizwa na wafamasia na zile zilizoandikwa na madaktari ikilinganishwa na fomu za wagonjwa zilizotoa maelekezo ya aina ya dawa".

Brigedia Mbungo amesema watuhumiwa hao wanaendelea kuhojiwa na kwamba mahojiano yakikamilika hatua za kisheria zitafuatwa.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu