
Salima Mdee Mbunge wa Kawe na Spika Ndugai
Kupitia vikao vya Bunge ambavyo ameviendesha leo Mei 15, 2020, Bungeni jijini Dodoma Spika Ndugai ameendelea kusema kuwa, hajaikubali hotuba hiyo kwa kuwa mwandishi wa hotuba hiyo ni Mbunge Halima Mdee na hayupo ndani ya Bunge.
"Hotuba ya kambi rasmi hatujaikubali sababu mwandishi wake ni Halima Mdee ni kati ya wale waliojifukuza wenyewe Bungeni, kwamba roho zao ni muhimu kuliko wengine, haiwezekani ukapitishia dirishani kazi zako zikafanyika, wakati wewe hata uliko hakujulikani" amesema Spika Ndugai
"Hotuba ya kambi rasmi hatujaikubali sababu mwandishi wake ni @halimamdee ni kati ya wale waliojifukuza wenyewe Bungeni, kwamba roho zao ni muhimu kuliko wengine, haiwezekani ukapitishia dirishani kazi zako zikafanyika, wakati wewe hata uliko hakujulikani"- Spika Ndugai.#Bungeni pic.twitter.com/FpqqN6mmdL
— EastAfricaRadio (@earadiofm) May 15, 2020
Mapema leo Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, alitoa waraka juu ya kuwataka Wabunge wake ambao walitekeleza agizo la kukaa Karantini kwa siku 14 warejee Bungeni kuanzia leo.