Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Siwezi kumlazimisha Sugu anikabidhi ofisi"- Tulia

Jumatatu , 23rd Nov , 2020

Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Dk. Tulia Ackson, ameanza utaratibu wa kusikiliza kero za wananchi, ambapo kila Alhamisi atakuwa anasikiliza kero mbalimbali katika ofisi yake iliyoko kwa mkuu wa wilaya ya Mbeya na kila Jumamosi atakuwa kwenye ofisi zake zilizopo Uyole.

Kushoto ni mbunge wa Mbeya Mjini kupitia CCM, Dkt. Tulia Ackson, na kulia ni mbunge mstaafu wa jimbo hilo kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi (Sugu).

Dkt. Tulia ameitoa hii leo Novemba 23, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake, na kusema kuwa hiyo ni moja ya ahadi yake aliyoitoa wakati wa kampeni kwamba atahakikisha anatenga muda wa kukutana mwananchi mmoja mmoja ili asikilize kero zake.

"Nimeanza utaratibu wa kusikiliza kero za wananchi wangu kila mwenye shida yeyote afike kwa kulingana na siku nilizozianisha," amesema Dkt. Tulia.

Akizungumzia suala la kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kupitia CHADEMA, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Sugu, Dk. Tulia, amesema kuwa hakuna chochote kilichofanyika kati yake na mtangulizi wake huyo aliyekuwa anatumia Ofisi za Ardhi.

"Hadi sasa hakuna makabidhiano na mbunge mstaafu, Joseph Mbilinyi, siwezi kumlazimisha, mimi nimejiandaa kikamilifu kuwatumikia wananchi siwezi kusubiri kwa sababu naona hajihusishi na chochote na ni mlolongo mrefu, ndiyo maana hata ofisi natumia nyingine", ameongeza Dkt.Tulia.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali