Jumapili , 4th Jun , 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene, amesema kwenye utumishi wa umma sio sehemu ya kuvuna utajiri na kujilimbikizia mali bali ni kwa ajili ya kutoa huduma bora kwa umma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene

Rai hiyo ameitoa leo wakati wa mahafali ya 37 ya chuo cha utumishi wa umma yaliyofanyika Jijini Tanga amesema kuwa ukiona mtumishi wa umma ni tajiri ujue huyo lazima ni fisadi au anatumia ofisi za umma Kwa ajili ya manufaa yake binafsi .

Aidha amekitaka chuo hicho kujikita katika kufanya tafiti ambazo zitawasaidia viongozi kuja na mikakati ya kumaliza changamoto ya ukiukwaji kwa maadili wa baadhi ya watumishi wa sekta hiyo.