Mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha ADA TADEA, John Shibuda
Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Maswa, Mkoani Simiyu kwenye uzinduzi wa kampeni zake Shibuda ,ameweka wazi kuwa hawana tataizo na vyama vingine vya siasa nchini.
“Sisi kama Chama cha ADA TADEA hatuna tatizo lolote na vyama vingine vya siasa bali tatizo letu kubwa ni mapambano dhidi ya madhira matatu ambayo ni; ujinga, maradhi na umaskini, na vita ya chama chetu ni kuhakikisha kuwa utawala bora unapatikana” alisema Shibuda
Aidha Shibuda amesema kuwa endapo chama hicho kitapewa ridhaa na watanzania kimejipanga kuhakikisha kinaondoa maadui wakubwa wa ustawi na maendeleo ya jamii nchi huku akiwasisitiza watanzania kumpigia kura za ndio katika nafasi ya urais.
Chama cha ADA TADEA kimezindua rasmi kampeni zake kitaifa mkoani Simiyu wilayani Maswa tarehe 27/09/2020 na kimetaja utawala wa sheria na siasa safi kuwa moja ya vipaumbele vyake.