Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yawalegezea wenyeviti wa mitaa

Jumanne , 17th Jan , 2017

Serikali imesitisha agizo lake lililokuwa linawataka wenyeviti wa Serikali za Mitaa kote nchini kurudisha mihuri katika Halmashauri za Wilaya na kuwapatia Watendaji wa Mtaa kuitumia mihuri hiyo katika shughuli mbalimbali za utendaji katika ngazi hiyo

George Simbachawene - Waziri wa TAMISEMI

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Waziri wa nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. George Simbachawene, amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa waendelee kutumia mihuri hiyo kama ilivyokuwa hapo awali mpaka pale utaratibu mwingine utakapotangazwa na kwamba uamuzi huo utawashirikisha ili kuleta ufumbuzi wa matumizi ya mihurio hiyo.

Mhe. Simbachawene amesema, hapo awali serikali ilikuja na uamuzi huo kama suluhisho la kuondokana na tabia ya wenyeviti wa serikali za mitaa wasio waadilifu ambao wanatumia mihuri hiyo vibaya kwa kuuza mali na mashamba ya kijiji, na wakati mwingine kupelekea migogoro mikubwa ya ardhi hapa nchini ikiwemo ya wakulima na wafugaji, na kutoa ardhi kwa wawekezaji kinyume cha sheria.

Aidha, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Halmashauri ya Ubungo na Kinondoni ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwongozo Bw. James Ngoitanile amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa kote nchini kutofurahia kurudishiwa mihuri hiyo na badala yake wapime utendaji wao na kuondoa kasoro zote zinazolalamikiwa.

HABARI ZAIDI

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali

Daktari wa GGML aliyebobea katika magonjwa yatokanayo na kazi, Cretus Karwan akimpatia vipimo mmoja wa wananchi waliotembelea banda la GGML na kupatiwa huduma za awali za upimaji wa afya katika maonesho ya OSHA yanayoendelea jijini Arusha.

Wananchi 200 wapimwa afya maonesho ya OSHA

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhoka akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Mwandamizi wa masuala ya jamii na maendeleo ya kiuchumi kutoka GGML, Ruth Mharagi alipotembelea banda la GGML katika maonesho ya afya na usalama mahali pa kazi jijini Arusha.

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu