Hayo ameyasema mwenyekiti wa Jamuhiya ya wafanyabiashara wa mafuta nchini TAPSOA bwana Farough Baghozah kwenye mahojiano maalumu nakuongeza kuwa kama serikali itaweka mpango huo itasaidia sana katika kuongeza soko la bidhaa hiyo nakupunguza ukame wa mafuta nchini.
Wameiomba serikali ielewe kuna asilimia kubwa ya wafanyabiashara wa mafuta sio waingizaji wa mafuta na kama itatokea upungufu wa mafuta basi inaweza sababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa bidhaa hizo.




